ARSEN WENGER ALA MWELEKA NI BAADA YA KIPIGO CHA 5–1 KUTOKA KWA LIVERPOOL

Arsene Wenger jana alipatwa na majanga mawili ya mwaka baada
ya kula mweleka muda mfupi baada ya timu yake ya Arsenal kupigwa 5-1 na Liverpool.
clip_image001Meneja huyo wa washika bunduki wa Uingereza alikuwa anawahi treni kurudi London katika mtaa wa Lime jijini Liverpool akiwa na wachezaji wake alipoteleza na kuanguka pwa!

Meneja huyo mwenye umri wa miaka 64 anaokenana pichani akiwa anaburuta begi lake wakati akiingia stesheni, lakini mara tu
baada ya kuvuka mlango wa kuingilia, anateleza na kula mweleka.

Mfaransa huyo aligumia kwa maumivu wakati askari polisi wawili walipofika kumsaidia. Msemaji wa Arsenal alinukuriwa baadaye
akisema kuwa mzee mzima hakuumia na hajambo.

Kama ulipitwa na Mechi hiyo Tazama Hapa Magoli hayo::

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post