“NILIUZA RAV 4 ILI NISHUTI VIDEO YA KUKERE, SASA NAENDESHA MAGARI YA 2013/2014” - IYANYA

IYANYA 1Alipoulizwa kwenye mahojiano na jarida la Yes juu ya gari lake la kwanza aina ya Rav4, Iyanya alisema…IYANYA 2“Ngoja nikwambie kitu, Mungu amenibariki na Range Rover ya 2010 na pia naendesha magari ya mwaka 2013 na 2014, ni baraka kwangu ila mimi sio kichaa sana wa magari. Bado nina Prado ambalo nimepewa hivi karibuni, bado pia nina kumbukumbu ya ile Rav 4 na natamani lingekuwepo kwenye gereji yangu ili niwe naliona kila siku.IYANYA 3Ngoja nisidanganye, ilifika kipindi nilihitaji kushuti video na nilikuwa sina hela. Ilikuwa ni Kukere. Nilitumia teksi kutembea mjini katika hali ya kuhakikisha video ya Kukere inatoka. Hivyo nilikuwa natumia taksi kila siku na watu walikuwa wakishangaa kuniona nimepanda gari zile ikiwa walijua ninaendesha Rav 4. Ilikuwa ni katika kuhakikisha watu wanaendelea kuniona kwenye tv na sio kunisahau”

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post