MSHINDI BALLON D'OR - CRISTIANO RONALDO….AWABWAGA MESSI & RIBERY!!

Usiku wa leo, huko Kongresshaus, Zurich, Nchini Switzerland, FIFA ilikuwa na Tafrija maalum ya kutunukia Watu mbalimbali Tuzo na Mchezaji Bora Duniani, alietwaa Tuzo ya FIFA Ballon d'Or ni…. CRISTIANO RONALDO….NI BORA DUNIANI!!!ARP3763283Hii ni mara ya Pili kwa Cristiano Ronaldo, ambae sasa anaichezea Real Madrid na ni Nahodha wa Nchi yake Portugal, kutwaa Tuzo hii na mara ya kwanza ilikuwa ni Mwaka 2008 wakati akiwa na Manchester United.ARP3763143Kwa kutwaa Tuzo, Ronaldo amewabwaga Lionel Messi, Mshindi kwa Miaka minne iliyopita, na Franck Ribery wa France na Klabu ya Bayern Munich.ARP3763238Nae Lejendari wa Soka Duniani kutoka Brazil, Edson Arantes do Nascimento ' Pele', ambae hakuwahi kutwaa Ballon d'Or kwa vile tu enzi zake ilikuwa ikipewa kwa Wachezaji wa Ulaya tu, leo amepewa Tuzo Maalum ya FIFA.

Akiipokea, Pele, huku akitokwa Machozi, alinena: “Niliahidi Familia yangu sitatokwa na Machozi lakini nimeshindwa kujizuia. Kwanza namshukuru Mungu kwa kunipa afya ya kucheza Miaka mingi. Nilikuwa na wivu na wale waliokuwa wakitwaa Ballon d'Or kwa sababu sikushinda, kwa sababu sikucheza Ulaya . Sasa nina Kombe langu!”

**KIBWAGIZO:

Kabla ya leo, haijawahi kutokea Mchezaji kutoka Bundesliga au Ligue 1 ya France akawemo kwenye FIFA/FIFPro Kombaini ya Dunia

Kwa Mwaka wa Pili mfululizo, hamna Mchezaji wa Ligi Kuu England kwenye Timu hii ya Dunia na Wachezaji wa Manchester United, Nemanja Vidic na Wayne Rooney, ndio walioteuliwa kwa mara ya mwisho Mwaka 2011.

Sergio Ramos: Kadi za Njano 142 na Kadi Nyekundu 18 lakini YUPO KIKOSI CHA DUNIA!

WASHINDI WA TUZO MBALIMALI:

FIFPRO WORLD XI

KIPA:

Manuel Neuer (Bayern Munich and Germany)

MABEKI:

Dani Alves (Barcelona and Brazil)

Philipp Lahm (Bayern Munich and Germany)

Thiago Silva (Paris St-Germain and Brazil)

Sergio Ramos (Real Madrid and Spain)

VIUNGO:

Xavi (Barcelona and Spain)

Andres Iniesta (Barcelona and Spain)

Franck Ribery (Bayern Munich and France)

MASTRAIKA:

Cristiano Ronaldo (Real Madrid and Portugal)

Zlatan Ibrahimovic (Paris St-Germain and Sweden)

Lionel Messi (Barcelona and Argentina)

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Tuzo ya Rais

Jacques Rogge, Rais wa zamani wa Kamati ya Kimataifa ya Olimpiki

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Kocha Bora Timu za Wanawake

Silvia Neid [Germany]

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Kocha Bora Timu za Wanaume

Jupp Heynckes [Bayern Munich-kabla hajastaafu Mwezi Mei]

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Tuzo ya Uchezaji wa Haki

AFGHANISTAN: Nchi iliyokumbwa na Vita kwa muda mrefu

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Tuzo ya Puskas [Goli Bora]

Zlatan Ibrahimovic [Kwa Goli la Tikitaka aliloifunga England]

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Tuzo Maalum

Edson Arantes do Nascimento ' Pele'

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Mchezaji Bora Kinamama

Nadine Angerer (Kipa wa Germany)

++++++++++++++++++++++++++++

FIFA Ballon d'Or

CRISTIANO RONALDO

source: soka in bongo

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post