KAMPUNI YA APPLE YAZINDUA iPad YA AJABU, BOBYA HAPA KUJUA ZAIDI

clip_image001Kampuni ya Apple ambayo ni kampuni maarufu sana hapa Duniani kutokana na ubora wa bidhaa zake, imeendelea kutisha katika ulimwengu wa teknolojia baada ya kuzindua iPad yenye umbo dogo zaidi ya hizi tulizo zoea kukutana nazo mtaani, Hata hivyo iPad hiyo haina tofauti kubwa sana kiutendaji na iPad nyingine, ila kinachofanya iwe ya pekee ni mwonekano wake na wembaba wake.
Angalia baadhi ya Picha zinazoonesha bidhaa hii mpya ambayo tayari ipo sokoni tangu mwishoni mwa mwaka jana na inapatikana kwa  bei ya kuanzia dola 500 za kimarekani na zaidi. clip_image001[6]Mara baada ya uzinduzi huu, Kampuni ya Apple inafikiria kutafuta jina lingine la bidhaa hii kutokana na upekee huo. Kazi kwenu mnaopenda kwenda na wakati, Haya tengeni hizo dola 500 au zaidi ili mjipatie mara zitakapo fika hapa bongo au fanyeni utaratibu wa kuzinunua online, Ikumbukwe kuwa zunapatikana kwa rangi mbili ambazo ni nyeupe na nyeusi.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post