JUAN MATA ANAINGIA, WILFRED ZAHA ANATOKA MANCHESTER UNITED. SOMA HABARI KAMILI

clip_image001Mchezaji wa Manchester United Wilfried Zaha imeripotiwa kuwa anakamilisha uhamisho wake wa mkopo kwenda Cardiff City kwa kipindichote cha msimu uliobakia.

Zaha, ambaye alijiunga na United akitokea  Crystal Palace kwa uhamisho wa 15 million-pound mwaka jana, amefanyiwa vipimo vya afya na timu hiyo inayofundishwa na mshambuliaji wa zamani wa United Ole Gunnar Solskjaer.

Gazeti hilo limeandika kuwa mchezaji huyo ameonekana akiingia kwenye hospitali huko Cardiff kwa ajili ya kufanyiwa vipimo. anategemewa kwamba ataweza kuanza katika mchezo wake wa kwanza na Cardiff dhidi ya Norwich City mnamo Feb. 1.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post