BREAKING NEWS:: MWANAMKE ANASWA NA MADAWA YA KULEVYA UWANJA WA NDEGE JIJINI DAR

1475804_640258869371444_352450160_nMWANAMKE Mtanzania, Salama Omari Mzale, amekamatwa jana- katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam akisafirisha dawa za kulevya kwenda nchini China.
Hadi leo saa nane mchana amekwishatoa kete 27 kwa njia ya haja kubwa.
Mwanamke huyo mkazi wa Mbagala Kongowe, anaendelea kutoa kete hizo katika vyoo vya Uwanja wa Ndege.
============
UPDATE:
Hadi saa 1 jioni (mida ya Tanzania); mwanamke huyu amekwishashusha kete 63!
============
Rai yangu:
Mwanamke huyu abanwe kisawasawa ataje alikoupata mzigo na huko ulikotoka ufuatiliwe hadi chain nzima iweze kujulikana na umma ujue hatma ya wahusika.

Tumeshachoka!

ORIGINAL SOURCE:: Jamii Forum

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post