KUMBUKUMBU YA SHARO YAJA, MSANII SHERRY KUMSOMEA DUA SIKU HIYO

clip_image002
Na Hamida Hassan
IKIWA anakaribia kufikisha mwaka mmoja tangu afariki dunia, marehemu Hussein Mkiety ‘Sharo Milionea’, dua maalumu ya kumbukumbu inatarajiwa kusomwa Novemba 26, mwaka huu.

Akizungumza na Risasi Mchanganyiko hivi karibuni jijini Dar es Salaam, mchekeshaji wa kike, Sherry Magali, alisema ameandaa dua itakayosomwa nyumbani kwake Mabibo, Dar siku hiyo kwa sababu pia ni siku yake ya kuzaliwa.
“Mimi na Sharo tunashea siku ya kuzaliwa. Sharo amefariki siku yake ya kuzaliwa, kwangu mimi nimeona ni vyema kufanya dua hii muhimu kwa lengo la kumkumbuka mwenzetu,” alisema Sherry.
source: Globalpublishers.info


Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post