Msikiti mkubwa wa Answar Sunna uliopo barabara ya saba mjini Dodoma umewaka moto mchana wa leo ikiwa ni muda mfupi baada ya swala ya mchana kumalizika....
Akiongea kwa njia ya simu toka Dodoma shuhuda wa tukio hilo amedai kuwa chanzo cha moto huo ni moto wa JIKO la wakazi wa ghorofa ya juu ya jengo la msikiti huo...Kwa mujibu wa shuhuda wetu, moto huo umefanikiwa kudhibitiwa na jeshi la zima moto na kwamba hakuna mtu aliyepoteza maisha kutokana na moto huo.
Taarifa na Picha na Rama Ngozi Dodoma NA AHMAD MACHAKU
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.