TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI KUHUSU MAJERAHA YA SHEIK PONDA ISA PONDA
dar es salaam 12/8/2013
sheikh ponda issa ponda (54) alipokelewa hapa ytaasisi ya ya tiba ya mifupa na upasuaji wa mishipa ya fahamu MOI jana tarehe 11/8/2013 saa 7.30 adhuhuri akitokea hospitali ya taifa muhimbili
baada ya kupokelewa alionekana akiwa na majeraha chini ya
bega la mkono wa kulia lililokuwa limeshonwa mbele na nyuma
madaktari wetu walifanya uchunguzi na kushauri afanyiwe kipimo cha x-ray ili ubaini kama kuna mvunjiko kwenye sehemu ya jeraha
tathimini ya madactari baada ya kupata majibu ya x/ray ilionyesha alikuwa na mvunjiko bila mifupa kupishana.
Vivyo hivyo kidonda hakikuwa katika hali nzuri licha ya tiba ya mwanzo na iliamuliwa afanyiwe upasuaji mpya ili kuzuia maambukizi kama kingeachwa hivyo
KWA HIYO ....
1-kufwatana na tiba ya awali aliyopata ikiwa ni pamoja na kushonwa jeraha kabla ya kufikishwa moi imekuwa vigumu kujua kama jeraha lilisababishwa na kitu gani
2-kipimo cha x-ray kilionyesha kwamba alikuwa amepata mvunjiko wa mfupa mkubwa wa bega bila mifupa kupishana
3-hivyo basi sheikh ponda issa ponda anaendelea n matibabu baada ya upasuaji .
Mkurugenzi mtendaji
Taasisi ya mifupa na upasuaji wa mishipa ya fahamu MOI
SOURCE:HABARIZUTULEO
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.