Dereve wa Isuzu Carry akiwa amepasuka eneo la kichwa baada ya abiria kumshushia kipigo, wakati ilipotokea ajali baina ya Basi la Abiria la ZAM ZAM linalofanya route ya Ruangwa – Dar es salaam na Isuzu Carry Eneo la Mnazi Mmoja Mjini Lindi.
Abiria wakiwa wameshuka na Kuja Kumchomoa Dereva wa Isuzu carry Na kuanza kumpa kichapo Hadi pale Mpashaji wa Habari hii alipowaambia kuwa waache kumpiga la sivyo atawachukulia hatua za kisheria huku akionekana kuwapiga picha, hiyo ikawa nafuu kwa Dereva huyo kuacha kupokea kipigo
Mmoja wa abiria wa Basi hilo akizozana na abira mwenzake katika eneo hilo la tukio. Basi hilo likitokea Dar es salaam Kuelekea Ruangwa leo hii na Limepata Ajali maeneo ya Mnazi Mmoja Lindi Mjini jirani na Mizani.
Tags
HABARI ZA KITAIFA