Unknown Unknown Author
Title: MAN UNITED KWA HASIRA SASA YAMGEUKIA GARETH BALE NA PAUNI MILIONI 60 MKONONI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Anayetakiwa: Gareth Bale (kushoto) amekuwa akihusishwa na kuhamia Real Madrid na sasa Manchester United KLABU ya Manchester United inaweza ...

clip_image001Anayetakiwa: Gareth Bale (kushoto) amekuwa akihusishwa na kuhamia Real Madrid na sasa Manchester United

KLABU ya Manchester United inaweza kugeuzia mawingo yake kwa Gareth Bale baada ya kumkosa mmoja wa wachezaji iliyokuwa inawataka sana.

Mabingwa hao wa Ligi Kuu wameshuhudia kiungo wa kimataifa wa Hispania chini ya umri wa miaka 21, Thiago Alcantara wa Barcelona akichagua kumfuata kocha wake wa zamani, Pep Guardiola klabu ya Bayern Munich.

Lakini United imedhamiria kumpa sapoti kocha wake mpya, David Moyes katika harakati zake za kuunda kikosi cha kutetea taji kwa kumnunulia winga wa Tottenham, Bale, ambaye alishinda tuzo tatu za Mchezaji Bora wa Mwaka msimu uliopita baada ya kufunga mabao 21 Spurs.clip_image001[6]Ameota mbawa: United ilikuwa inamtaka Thiago Alcantara (katikati), ambaye amesaini Bayern Munich

Beki kinda wa Uruguay, Guillermo Varela ni mchezaji pekee aliyesajiliwa na United majira haya ya joto, lakini klabu hiyo inaweza kuanza mpango wa kumsajili kwa Pauni Milioni 60 Bale mwezi huu, kwa mujibu wa Daily Mirror. 

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top