Unknown Unknown Author
Title: TAIFA STARS YAWASILI SALAMA MOROCCO TAYARI KWA MECHI JUMAMOSI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Taifa Stars imewasili leo hapa Marrakech, Morocco tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamo...

clip_image001Taifa Stars imewasili leo hapa Marrakech, Morocco tayari kwa mechi ya mchujo ya Kombe la Dunia dhidi ya wenyeji Morocco itakayochezwa Jumamosi- Juni 8 mwaka huu.

Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager imefikia hoteli ya Pullman ambayo pia ilifikia timu ya Ivory Coast ilipokuja kucheza na Morocco. Stars imetua na kikosi cha wachezaji 21 wakati Mbwana Samata na Thomas Ulimwengu watawasili kesho- Juni 4 mwaka huu saa 8 mchana wakitokea Maputo, Msumbiji ambapo jana- Juni 2 mwaka huu timu yao ya TP Mazembe ilicheza mechi ya Kombe la Shirikisho.

Mechi kati ya Stars na Morocco itachezwa kuanzia saa 3 usiku kwa saa za hapa ambapo Tanzania itakuwa saa 5 usiku.

Boniface Wambura

Ofisa Habari

Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF)

+212610120619

Marrakech, Morocco

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top