Unknown Unknown Author
Title: MAJAMBAZI WAWILI WANUSURIKA KUUAWA MKOANI LINDI LEO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga akionyesha silaha iliyokutwa kwa majambazi hayo. Jeshi la Polisi Mkoani Lindi linawashikil...

clip_image001Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga akionyesha silaha iliyokutwa kwa majambazi hayo.clip_image001[6]Jeshi la Polisi Mkoani Lindi linawashikilia watu wawili kwa Tuhuma za Unyanganyi kwa kutumia silaha na kujeruhi Mfanyabiasha wa Duka katika kijiji Cha Kitomanga Wilayani Lindi huku wakiwa katika hospital ya Mkoa baada ya kunusurika kufa kufuatia Wananchi wenye hasira kutaka kuwaua kwa kuwachoma Moto.

Akiongea na waandishi wa habari Ofisi kwake hii leo,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Lindi,George Mwakajinga alieleza kuwa Watuhumiwa hao waliojitambulisha kwa Rajabu Juma Mbete(26) mkazi wa manispaa ya Lindi na Hamis Athuman(32) mkazi wa Mbembetini Kibiti Mkoani Pwani licha ya kupora simu 6 na fedha taslim laki 6 pia walimjeruhi kwa Mapanga Bw Hamis Hassan Muuza duka hilo.clip_image001[8]Mwakajinga alibainisha kuwa Majambazi hayo yanayosadikiwa kuwa 4 walifanikiwa kukimbia baada ya Bunduki waliyokuwa nayo kugoma kufyetua risasi hali iliyofanya wanavijiji vya Kitomanga,Mkwajuni na Mbwemkuru kuanza msako na kufanikiwa kuwakamata na kuwajeruhi kwa kuwapiga na kuwachoma moto kabla hawajapata msaada wa Jeshi la Polisi.

Akielezea kuhusu kukutwa na risasi tatu za Shortgun,Bangi pamoja na Bunduki aina ya Shortgun ya kienyeji, Kamanda mwakajinga alifafanua Bunduki hiyo Ambayo hutumia risasi za Short gun pia walikutwa na risasi 3.clip_image001[10]Kufuatia kukamatwa kwa majambazi hao baadhi ya Wafanyabiashara Manispaa ya Lindi akiwemo Seif Nasor na Ahmaid Nachuli wameeleza kuwa tatizo la kuongezeka kwa majambazi kunachangiwa na Uozo wa sheria hali inayosababisha jamii kujichulia sheria mkononi.

Watuhumiwa hao ambao wamelazwa huku wakiwa chini ya Ulinzi wa Jeshi la Polisi watafikishwa mhakamani mara baada ya Afya yao Kuimarika kutokana kunusurika kuchomwa Moto na Wananchi ambapo tayari wameweza kutambuliwa na baadhi ya wanakijiji

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top