Nawashukuru sana ndg,jamaa na Marafiki kwa jinsi mlivyojitoa na
kumuombea Dua mtoto wangu Mpendwa Nuru Abdulaziz katika kipindi chote toka amezaliwa tarehe 05 march 2013 na alipoanza kuumwa na kuvimba upande mmoja wa kichwa na kulazwa katika hospital ya Mkoa wa Lindi tarehe 08 march, 2013. Hakika mlinifariji sana na kunitia Moyo...Kwa Mapendo ya Mungu yeye alimpenda zaidi na kuweza kumchukua tarehe 24 march na kuzikwa siku hiyo hiyo Kwa Niaba ya Familia yangu nawashukuru sana kwa subira mliyonipa na mnavyozidi kujitokeza kunifariji katika kipindi hiki kigumu..Mungu
awape baraka nanyi. Tuko pamoja kwa kila jambo
Ahsante.
Abdulaziz Ahmeid-Mwenyekiti wa Klabu ya Waandishi wa
Habari Mkoa wa Lindi au maarufu Abdulaziz Video wa Channel ten-Lindi
Tags
HABARI ZA KITAIFA