KENYA WAIFUATA UGANDA ROBO FAINALI TUSKER CHALLENGE


Beki wa Kenya, Abdallah Juma akimsukumia kitu cha mbavu Nahodha wa Ethiopia Fikru Teffera Lemessa katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge uliofanyika Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala, Uganda. Kenya ilishinda 3-1, mabao ya Ramadhan Mohamed Salim, Clifton Miheso na David Ochieng, wakati la Ethiopia lilifungwa na Gatech Panom Yietch. Kenya imeungana na Uganda kutinga Robo Fainali na sasa Ethiopia wataiombea Sudan Kusini ifungwe na Uganda katika mchezo unaofuata, ili wao wajaribu hata kuwania kupita kama mmoja wa washindi wa tatu bora. Kocha wa Tanzania Bara, Mdenmark Kim Poulsen akiwa na shabiki wa kike wa Tanzania wakati wanaangalia mchezo wa Kenya na Ethiopia.Katibu wa CECAFA, Nocholas Musonye wakati anaangalia mechi ya nchi yake, Kenya na EthiopiaRamadhan Mohamed Salim wa Kenya, akimtoka beki wa Ethiopia Mehari Mena Medelcho katika mchezo wa mwisho wa Kundi A, Kombe la Mataifa ya Afrika Mashariki na Kati, CECAFA Tusker Challenge uliofanyika Uwanja wa Mandela, Namboole mjini Kampala, Uganda. Kenya ilishinda 3-1, mabao ya Ramadhan Mohamed Salim, Clifton Miheso na David Ochieng, wakati la Ethiopia lilifungwa na Gatech Panom Yietch. Kenya imeungana na Uganda kutinga Robo Fainali na sasa Ethiopia wataiombea Sudan Kusini ifungwe na Uganda katika mchezo unaofuata, ili wao wajaribu hata kuwania kupita kama mmoja wa washindi wa tatu bora.Anthony Kimani akimtoka Mehari Mena Medelcho
Previous Post Next Post