Mratibu wa Miss Kinondoni 2012, Vivien Sirikwa (kushoto) akizungumza na Waandishi wa Habari leo katika ukumbi wa mikutano wa Serengeti, jengo la Benjamin Mkapa, Mtaa wa Azikiwe, Dar es Salaam wakati wa kutaja tarahe ya shindano la mwaka huu, ambayo ni Septemba 14, kwenye ukumbi wa Cassa Complex, Mikocheni, Dar es Salaam. Kulia ni Victoria Kimaro, Meneja wa Redd’s, wadhamini wakuu wa Miss Kinondoni 2012.Washiriki wa Miss Kinondoni 2012, kutoka kushoto ni Mahma Said, Brigitte Alfred, Esther Mussa, Zulfa Vuai, Diana Hussein, Irene David, Jennifer Manu, Kudra Lupatu, Judith Sangu na Mwantumu Mustafa wakiwa katika picha ya pamoja wakati wa kutambulishwa leo, kwenye ukumbi wa Serengeti, jengo la Benjamin Mkapa, tayari kwa kushinda lao litakalofanyika Septemba 14, mwaka huu. Katika shindano hilo, mshindi ataondoka na seti ya vifaa vya sebuleni vyenye thamani wa Sh. Milioni 5, wa pili jokofu la ukubwa wa familia, lenye thamani ya Sh. Milioni 3, wa tatu TV ya ubapa ya nchi 32, yenye thamani ya Sh. Milioni 1.5, wa nne Sh. 500,000 na wa tano Sh. 300,000 wakati wengine kila mmoja atapatya kifuta jasho cha Sh. 100,000.
wafuatao ni washiriki wa shindano hilo.
MAHMA SAIDI BRIGITTE ALFRED
ESTHER MUSSA ZULFA VUAI
DIANA HUSSEIN IRENE DAVID
JENNIFER MANU KUDRA LUPATU
JUDITH SANGU MWANTUMU MUSTAFA