Unknown Unknown Author
Title: HII NDIO KAULI YA SAGNA KUHUSU CLUB YA ARSENAL
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mchezaji wa Arsenal Bacary Sagna amekubali kwamba yuko tayari kuongea na club yake ili kuongeza mkataba lakini bado haelewi kwa nini club hi...

Mchezaji wa Arsenal Bacary Sagna amekubali kwamba yuko tayari kuongea na club yake ili kuongeza mkataba lakini bado haelewi kwa nini club hiyo imemuuza mtu kama Alex Song.

Sagna mwenye miaka 29 ya pumzi akiwa anakaribia kurudi kwenye nyasi baada ya kujeruhiwa msimu uliopita amekiri kwamba ana hofu ya maisha ya club yake ya arsenal na sasa ni wazi anatarajia kila msimu arsenal itakua inauza wachezaji.

Kuhusu Van Persie kuuzwa, Sagna anasema alitarajia kabisa kwa sababu ilishajulikana na wachezaji wengi wa Arsenal ni kama kuna kitu kilikua kinaendelea lakini kitu ambacho Sagna hakukitegemea ni kuuzwa kwa Alex Song, ilikua surprise kwa sababu alikua na miaka mitatu imebaki kwenye mkataba wake, hapo Sagna anasisitiza kwamba haelewi kwa nini imetokea kwa song na ni hasara kubwa kwa club.

Namkariri akisema “inapotokea wachezaji wawili waliofanya vizuri msimu uliopita wanaondoka, ni lazima kuwe na maswali mengi, wakati mwingine mtaani nakutana na mashabiki wanaongea na mimi, naelewa wamekasirika, mimi pia nimekasirika”

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top