Zuma aowa tena na kuvalia vazi la kijadi

Rais Jacob Zuma

Rais Jacob Zuma wa Afrika Kusini ameoa mke wane, kwenye sherehe ya jadi ambapo wake zake wengine watatu piya walihudhuria.

Bwana Zuma, mwenye umri wa miaka 70, alivaa ngozi ya chui na kubeba mkuki na ngao, mavazi ya jadi ya Kizulu, kwenye harusi iliyofanywa jimbo la KwaZulu-Natal.

Wakuu wanasisitiza kuwa Bwana Zuma mwenyewe anagharimia sherehe hizo za wikiendi hii.

Bi arusi, Bongi Ngema, amefuatana na Rais Zuma kwenye ziara zake rasmi kwa miaka kadha.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post