NIJUZE NIJUZE Author
Title: MIMBA ZA UTOTO NI TATIZO LINDI.
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Umaskini uliokithiri miongoni mwa wazazi na walezi pamoja na  mila  na desturi zilizopitwa na wakati  kumeelezwa  kuwa  ni chanzo cha kuong...

What-Not-To-Do-When-Pregnant Umaskini uliokithiri miongoni mwa wazazi na walezi pamoja na  mila  na desturi zilizopitwa na wakati  kumeelezwa  kuwa  ni chanzo cha kuongezeka  kwa tatizo  mimba za utoto mkoani Lindi
Hayo yamebainishwa w kwenye mkutano  wadau wa afya ya uzazi na stadi za  maisha ulioendeshwa  na shirika lisilo la kiserikali  Wanawake na Maendeleo (WAMA) kwa  kushirikiana  na Engenderhealth kwa ufadhili wa USAID uliofanyika  kwenye ukumbi  wa  mikutano ofisi ya mkuu wa mkoa jana.
Akizungumza  kwa  niaba  ya washiriki wengine  afisa utamaduni katika Manispaa ya Lindi Maneno Juma  alisema kutokana kukithiri kwa  umaskini  wazazi wengi  wanashindwa kuwathibiti  mabinti  zao  kwa vile huwatumia hao kuwa chanzo  cha  mapato  kwa ajili  ya kuendesha familia.
Alisema  kuwa  kutokana  na wazazi  kushindwa kukemea vitendo vichafu ikiwemo kushiriki mapenzi  vinavyo fanywa  na mabinti  zao wakiwemo mapenzi  kwa  wanafunzi  wa shule za sekondari  na hivyo  kusababisha kupata mimba  wakiwa kwenye umri mdogo.
Alisema  wazazi  na walezi  wamekuwa  na tabia  ya kutokemea vitendo vya Watoto  kutoka nyumbani nyakati za usiku  na kurudi asubuhi  wakiwa  na  zawadi mbalimbali na fedha ambazo uwaziba midomo washindwe kukemea tabia hiyo chafu.
Nae Fatuma Shomali alisema  wazazi au walezi  wengi siku hizi wameacha kufuata  maadili ya dini na mila ya kukaa pamoja  na Watoto wao wa kike  kwenye moto ya jioni na  kuwafunda kwa kuwakanya kutenda matendo  yasiyo kuwa yenye  maadili  mema.
Shomali  alisema pia wazazi hao  wanashindwa kutumia  nafasi ya  uzazi kwa kuwakemea  Watoto wengine ambao sio  Watoto wao pale wanapowakuta  wanatenda matendo yasiyo fuata  maadili mema.

MWANJA IBADI Lindi

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top