NIJUZE NIJUZE Author
Title: MANISPAA YA LINDI WANAONYESHA KUJALI
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
WATU wa tano  kati ya 426  wa Manispaa  ya Lindi  waliopata huduma ya  upimaji  virusi  vya ukimwi kwa hiari  pamoja na huduma ya  mpango ...
lindi_map2 WATU wa tano  kati ya 426  wa Manispaa  ya Lindi  waliopata huduma ya  upimaji  virusi  vya ukimwi kwa hiari  pamoja na huduma ya  mpango wa uzazi kutoka shirika  lisilo kuwa la kiserikali la Mariestopes wamebainika kuambukizwa  virus vya ukimwi( VVU).
Hayo yamebainishwa  na  afisa mradi wa elimu rafiki  kwa  vijana Diana Karioki  wa shirika la Mariestopes tawi la Mtwara wakati alipokuwa anafanya  majumuhisho  baada ya  kukamilika  kwa utoaji  wa  huduma  za  uelimishaji vijana , upimaji  wa  virusi vya ukimwi na huduma za mpango wa uzazi uliofanyika katika  kata tano  za manispaa  hiyo.
Diana alisema kuwa  katika  kipindi  cha siku tano baada ya uzinduzi waliweza kuwafikia wanawake 366 ambao  walipata huduma za uzazi  wa mpango na upimaji virusi vya ukimwi .
Alisema Wanawake  297 walipata huduma  ya uzazi wa mpango  na 147 walichagua  huduma ya vipandikizi ambavyo  hudumu kwa miaka  mitatu, 91 huduma ya sindano na  59  walipata  vidonge.
Afisa  mradi  huyo  alisema kati ya watu 250 waliojitokeza kupima ukimwi pekee  190 walikuwa  wanawake  ambapo watano kati yao walibainika kuambukizwa na virusi vya ukimwi,  na wanaume 60  walikuwa ni salama.
Alisema vijana ambao ndiyo walengwa katika mradi huo hawakujitokeza kwa wingi kama ilivyotazamiwa kutokana kutokuwa na elimu ya kutosha juu ya elimu rafiki kwa vijana inayoendeshwa na mariestopes.
Kwa  mujibu wa taarifa mratibu  wa  ukimwi  mkoa wa Lindi Magege s magege kutokana na  utafiti wa  viashiria vya  ukimwi  na  malaria  kwa kipindi cha mwaka 2007/08 kuwa kiwango cha  maambukizi  ya ukimwi mkoani  humo yako  kwa asilimia 3.8 wakati  manispaaa ya Lindi  inaongozwa kimkoa kwa asilimia 8.9.
Magege alisema kuwa  wilaya inayofuata kwa  maambukizi ni  Ruangwa 3.8  Nachingwea  kwa asilimia 3.6 Liwale 2.3 Kilwa 2.3 na Lindi  ni asilimia 2.0.

Mwanja Ibadi Lindi

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top