Taarifa za uhakika zilizotua hivi punde kutoka mkoani Arusha zinadai kuwa mahakama kuu kanda ya Arusha imetoa hukumu ya kesi ya kupinga matokeo katika jimbo la Arusha Mjini na kutengua ubunge wa mbunge wa jimbo hilo Godbless Lema .
Hivyo kwa sasa jimbo hilo halina mbunge baada ya mbunge wake Lema kushindwa kesi hiyo ya kupinga matokeo ya uchaguzi mkuu uliofanyika mwaka 2010.
Tags
Siasa Ya Tanzania