Umesema kuwa endapo fedha zitokanazo na Mifuko ya NHIF, CHF na fedha za papo kwa papo zitasimamiwa vyema na kutumiwa katika ununuzi wa dawa, tatizo la ukosefu wa dawa vituoni litapungua na kuondoa malalamiko kwa wananchi.
Mkurugenzi Mkuu wa mfuko huo Bw Emanuel Humba alieleza Wadau wa mfuko huo kuwa suala la ukosefu wa dawa vituoni lichukuliwe kama changamoto katika miaka 10 ya NHIF
"Jamani Mfuko wetu hauna jukumu la kusambaza dawa na hatuwezi kuingilia kamwe majukumu ya MSD, ila tunachowashauri ni kutumia vizuri fedha za vyanzo vingine kununulia dawa wakati kunapoonekana upungufu wa dawa kutoka MSD," alisisitiza.
Aidha HUMBA alisema kuwa mchango mkubwa unaofanywa na NHIF katika kuhakikisha huduma za matibabu zinakuwa bora ni utoaji wa mikopo ya vifaa tiba na ukarabati wa majengo ambayo itaviwezesha vituo kuboresha huduma zake ambazo zitakuwa ni kwa wananchi wote na si kwa wanachama peke yake.
| Mkurugenzi mkuu NHIF,Emanuel Humba |
Wadau hao wakichangia mada zilizowasilishwa na viongozi wa NHIF, walisema kuwa moja ya mambo yanayokwamisha wananchi kujiunga na CHF ni ukosefu wa dawa na huduma mbovu vituoni ambapo walishauri kuwa wakati uhamasishaji ukiendelea ni vyema na matatizo hayo yakashughulikiwa ili wananchi wawe na imani zaidi.
Pamoja na kuonekana kuwepo kwa changamoto zinazokwamisha suala hilo,Kaimu Mkuu wa Mkoa wa Lindi,Magalula Saidi Magalula wakati akifungua mkutano huo wa wadau kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa huo Ludovick Mwananzira, alizitaka Halmashauri kujipanga na kuweka mikakati ya kukabiliana nazo lakini pia kuweka sheria itakayowalazimisha wananchi kujiunga na CHF.
| Magalula Saidi Magalula, |
Mkutano huo wa Wadau wa Mfuko toka Mkoa wa Lindi ulitanguliwa na utoaji wa Msaada wa Mashuka katika wadi za Hospital ya Mkoa ( Sokoine Hosp)na kukabidhi Sare za usalama wa Madereva wa Bodaboda
Tags
Lindi