Rais wa Tanzania Jakaya Kikwete aliueleza mkutano wa mwaka wa makamanda na maofisa wa polisi kuheshimu haki za binadamu wakati wa utekelezaji wa kazi zao, The Citizen la Tanzania liliripoti Jumanne (tarehe 6 Machi).Kikwete katika hotuba yake, alinukuu ripoti za matumizi makubwa ya nguvu kwa watuhumiwa, na kueleza masikitiko kuhusu ongezeko la malalamiko kutoka kwa wananchi. "Ninataka mlijadili hili na kutafuta njia za kulimaliza," Kikwete alisema Jumatatu. "Ikiwa ni pamoja na suala la nidhamu katika mitaala ya vyuo vya mafunzo ya polisi," aliongeza.
Kauli ya Kikwete ilikuja wakati idadi ya maofisa wa polisi waliripotiwa kwa kutuhumiwa kwa utovu wa nidhamu. Kikwete alitumia mfano wa ofisa wa polisi huko Moshi ambaye alitiwa mbaroni kwa kuacha kituo chake, akikutwa katika ukumbi wa disko akiwa na bombomu yenye risasi.
Rais alisema polisi walio wengi ni waaminifu, na kuwaagiza maofisa kutokomeza rushwa na kuwafukuza maofisa watakaopatikana na makosa ya kuvunja sheria. Rushwa hiyo inaleta kutoaminiwa kwa polisi miongoni mwa wananchi, alisema