BREAKING NEWS: BOBAN AMPIGA VICHWA OKWI BAADA YA KUFUNGWA NA YANGA

Kufuatia matokeo ya kufungwa na watani wao wa jadi 1-0 dakika chache zilizopita, taarifa kutoka chanzo cha kuaminika kutoka ndani ya dressing room ya Simba SC ni kwamba Haruna Moshi Boban amempiga vichwa mchezaji mwenzie Mganda Emmanuel Okwi kwa madai ya kuikosesha ushindi timu kwa kukosa mabao mengi ya wazi.

“Haruna amempiga Okwi baada ya mechi kuisha huku akimtuhumu kuikosesha timu ushindi kwa kukosa kufunga katika nafasi za wazi.Baada ya kumpiga Okwi, Haruna ameondoka hapa uwanjani peke yake bila kuongozana na wachezaji wenzie,” kilisema chanzo cha habari.

Mpaka sasa haijajulikana Okwi ameumia kwa kiasi gani kutokana na kipigo alichokipata kutoka kwa Boban.

USHINDI WA YANGA DHIDI YA SIMBA KTK PICHA.... ALAMBAA! ALAMBAAA ! HUYU NI MZEE YUSUF MJUMBE WA KAMATI YA UTENDAJI YA YANGA

FADHILA LEMBA


Athuman Idd Chuji ( shoto ), Jackson Chove na Said Mohamed Mohamed Hussein ' Mmachinga ' ( shoto ), Steve Nyerere na Edibily Lunyamila ( kulia )

Kama wamemwagiwa maji vile

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post