NIJUZE NIJUZE Author
Title: Mashambulio mapya yaanza Libya
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Majeshi yanayomtii kiongozi wa Libya aliyeondolewa Kanali Muammar Gaddafi yameanza mashambulio mapya kwenye mji wa Bani Walid. Wanaomtii wa...

imageMajeshi yanayomtii kiongozi wa Libya aliyeondolewa Kanali Muammar Gaddafi yameanza mashambulio mapya kwenye mji wa Bani Walid.

Wanaomtii wamekuwa wakirusha makombora na kutumia wadunguaji kuyalenga majeshi yanayompinga Gaddafi kwenye lango la kaskazini la mji huo.

Majeshi yanayompinga Gaddafi yanasonga taratibu katika ngome nyingine ya wanomtii - mji wa pwani wa Sirte.

Wakati huo huo, baraza la mpito la taifa, uongozi wa mpito wa Libya, unajadili kuhusu baraza jipya la mawaziri.

Taarifa kutoka Bani Walid zinasema milipuko na milio ya risasi yamekuwa yakisiskika nyakati za asubuhi baada ya majeshi yanayomwuunga mkono Gaddafi kurusha makombora.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top