NIJUZE NIJUZE Author
Title: Ferguson aelezea nguvu za TV katika soka
Author: NIJUZE
Rating 5 of 5 Des:
Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema television zina nguvu kupita kiasi katika soka ya Uingereza. Amedai vilabu vimepotez...

Meneja wa Manchester United Sir Alex Ferguson amesema television zina nguvu kupita kiasi katika soka ya Uingereza.

Sir Alex Ferguson

Amedai vilabu vimepoteza udhibiti wa ratiba hali inayoathiri timu zinazocheza soka Ulaya.

Katika mahojiano yake ya kwanza na BBC tangu alipofuta kususia mahojiano na kituo hicho, Sir Alex amesema kwa sababu ya kiasi kikubwa cha pesa ambacho vituo vya televisheni huweka katika michezo, sasa wanaonekana kudhibiti kila kitu.

Alipoulizwa iwapo televisheni kwa sasa zina nguvu sana katika mchezo, alisema "Hakika - unaposhikana mikono na shetani huna budi kujiandaa na yatakayokukabili. Amevifananisha vituo vya televisheni sawa na Mungu kwa wakati huu na kumalizia kusema - ni wafalme.

Sir Alex pia alidai vilabu havina budi kupewa pesa zaidi kutoka vituo vya televisheni. Amesema wasimamizi wa Ligi Kuu ya soka ya England wameuza mechi kwa nchi 200 na akaongeza " unapofikiria hayo sidhani kama tunapewa fedha za kutosha".

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top