Seattle Sounders na Manchester Utd

image

Dakika 14 za MRISHO NGASSA

Binafsi nimefurahishwa na namna Ngassa alivyocheza, Sounders wanamtafuta mbadala wa winga wao Steve Zakuani aliyepata majeraha ya muda mrefu,

Moja kati ya sifa za mchezaji wa kuziba nafasi ya Zikuani anatakiwa awe na spidi, awe na movements nzuri akiwa au hana mpira, moja kati ya vitu vilivyonifurahisha kwa Ngassa ni hali ya kujiamini aliyokua nayo,tukumbuke kwanza Ngassa hakuwa mchezaji wa Sounders bali alipewa nafasi ili wampime uwezo wake kwenye mechi kubwa kama dhidi ya Man Utd,

Nilipata wasaha wa kufanya mahojiano na mkurugenzi wa ufundi wa SONDERS bwana Chris Henderson binafsi alivutiwa sana kipaji cha Ngassa.

Mpambano uliokuwa unasubiliwa kwa hamu na mashabiki wengi wa soka ulimwenguni kati ya Seattle Sounders na Manchester Utd umemalizika kwa Man Utd kufanikiwa kuichapa Sounders Mabao 7-0.

kutoka shafii.blogspot.com

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post