VIDEO: SNURA AONGELEA KUFANYA KAZI NA DON JAZZY..!

Kila mtu alilipokea kwa style yake hili suala la mtayarishaji na msanii mkubwa wa muziki barani Afrika Don Jazzy kujirecord video akiimba wimbo wa Chura wakwake Snura.Snura na Don Jazzy
Wapo ambao walilichukulia kama kawaida tu, ila pia wapo ambao walilichukulia kama hatua kwa muziki wa Bongo Fleva, na hivyo kitendo hicho kuwa kama surprise kwa wengi.

Lindiyetu.com imepiga story na Snura kujua vipi alikipokea kitendo hicho. Snura ametusanua kuwa sio mara ya kwanza kwa Don Jazzy kufanya hivyo, bali alikwisha wahi kupost clip ambayo Snura na team yake walikuwa wakicheza wimbo huo huo wa Chura. Na hivyo ni dhahiri kabisa kwamba mkali huyo wa Mavin anauzimia wimbo huo wa Chura.

Snura hajataka kupoteza wakati wala nafasi, ameamua kutembelea chaki kwa kuuachia uongozi wake kazi ya kutafuta connection na mwisho wa siku kufanya kazi na Don Jazzy kwakuwa anaamini kuwa Don Jazzy ni shabiki wake.

Play hii video hapa chini kumsikiliza Snura akielezea mchongo mzima.


++++++++++++++++++++++++++++++++++++++

++++++++++++++++++++++++++++++++++++++
KUWA KARIBU NASI LINDIYETU.COM
Usipitwe!! Ungana na Familia hii kupitia FacebookTwitter na Instagram ili kupata Infortainment zote!! Usikose kujiunga na Youtube channel yetu ili kupata Exclusive mbalimbali kali kutoka LindiYetu TV

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post