Unknown Unknown Author
Title: KWAHERI BONDIA THOMAS MASHALI (REST IN PEACE)
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Jina lake halisi ni Christopher Fabian Mashali ila jina la kazi ni maarufu kama Thomas Mashali .  Umaarufu wake umetokana na uwezo wak...
Jina lake halisi ni Christopher Fabian Mashali ila jina la kazi ni maarufu kama Thomas Mashali
Thomas Mashali
Umaarufu wake umetokana na uwezo wake wa kupigana akiwa ulingoni ambapo amewahi kupigana dhidi ya mabondia mbalimbali wa ndani na nje ya nchi.

Mashali ambaye alikuwa bado anahitajika kwenye tasnia ya ngumi Tanzania amefariki dunia katika Hospitali ya Taifa Muhimbili. 

Hadi sasa bado chanzo cha kifo chake hakijulikani huku matukio mchanganyiko yakihusishwa na kifo.
Thomas Mashali
Ripoti ya awali inasema Thomas Mashali amefariki kwa kupigwa na wananchi baada ya kuhusishwa na tetesi wa wizi.

Lakini upande mwingine umedai kuwa Mashali alikuwa kwenye ugomvi binafsi na mtu kabla ya kupigwa na kujeruhiwa eneo la Kimara huku ikielezwa kuwa alikuwa kwenye klabu cha pombe.

Mashali anayedaiwa kuvuja damu nyingi kabla ya kufikishwa hospitali, inasemekana kuwa hadi jioni ya ya jana alikuwa na bondia mwenzake, Francis Cheka

Baada ya tukio hilo la kupigwa huko Kimara Mashali alipelekwa katika Hospitali ya Sinza Palestina kabla ya kupelekwa Muhimbili ambako mauti ilimkuta.
Taarifa zaidi kuhusu msiba huu zinafuata hapahapa.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top