NGOMA, TAMBWE WAIPA POINT TATU YANGA SC DHIDI YA MWADUI FC

Young Africans
Ligi Kuu soka Tanzania bara imeendelea leo September 17 ambapo Mabingwa watetezi wa Ligi Kuu Tanzania bara Dar es Salaam Young Africans walisafiri wakitokea Dar es Salaam kwenda Shinyanga kuwafuata Mwadui FC kwao mechi ambayo imemalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa goli 2-0.

Yanga walianza kupata goli la 1 katika dakika ya 5 ya mchezo kupitia kwa mshambuliaji wa Hamis Tambwe ambapo goli hilo lilidumu mpaka kipindi cha pili kwenye mchezo huo, katika dakika za nyongeza Yanga walipata goli la 2 kupitia Donald Ngoma na kufanya mchezo huo kumalizika kwa Yanga kuibuka na ushindi wa 2-0 dhidi ya Mwadui FC.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post