Inapendeza pale wapenzi wanapokuwa katika tasnia moja mathalani ya muziki kama ilivyo kwa Jay Z na Beyonce ama ilivyokuwa kwa Rihanna na Chris Brown kwani husaidiana kwa ukaribu zaidi na kujengana kimuziki.

Waswahili husema “ndege wafananao ndio wanaoruka pamoja”, kuna kila sababu na uwezo wa mtu kuingia kwenye fani ambayo mtu wake wa karibu au mpenzi wake amepelekea yeye kuingia kwenye hiyo fani, Diamond Platnumz wakati Wema Sepetu alipokuwa mpenzi wake waliwahi kupanda jukwaani na kuimba wimbo kwa pamoja ingawa Wema hakuwahi kujihusisha na muziki.
Msanii wa Bongo Movie Flora Mvungi yeye aliingia kwenye muziki baada ya kuingia kwenye mapenzi msanii wa muziki H Baba, lakini pia H baba naye alianza kujihusisha na masuala ya muvi baada ya kuwa na mahusiano na Frola Mvungi.

Kajala Masanja ndiye aliyemfanya Quick Racka kuingia kwenye tasnia ya filamu kama ambavyo Steven Kanumba alivyomwingiza Wema kwenye tasnia ya filamu. Quick Racka amejaaliwa vipaji vingi ikiwemo uandishi wa mistari, uimbaji na hata uigizaji, kwa upande wake ameshindwa kumfanya mpenzi wake afuate nyayo za uimbaji.
Msanii wa Bongo Movie Flora Mvungi yeye aliingia kwenye muziki baada ya kuingia kwenye mapenzi msanii wa muziki H Baba, lakini pia H baba naye alianza kujihusisha na masuala ya muvi baada ya kuwa na mahusiano na Frola Mvungi.

Kajala Masanja ndiye aliyemfanya Quick Racka kuingia kwenye tasnia ya filamu kama ambavyo Steven Kanumba alivyomwingiza Wema kwenye tasnia ya filamu. Quick Racka amejaaliwa vipaji vingi ikiwemo uandishi wa mistari, uimbaji na hata uigizaji, kwa upande wake ameshindwa kumfanya mpenzi wake afuate nyayo za uimbaji.

Nini sababu ya yeye kushindwa? Yeye aliwezaje kuingia kwenye muvi? msikilize katika sauti hapo chini akitiririka.
Tags
HABARI ZA WASANII