HUU NDIO WIMBO WA PAPA WEMBA ALIOMSHIRIKISHA DIAMOND PLATNUMZ KABLA YA KUKUTWA NA UMAUTI WAKE

Wiki tatu kabla ya kifo cha Papa Wemba, Jumapili ya jana, Diamond alirekodi wimbo naye jijini Paris, Ufaransa.
Diamond featuring Papa Wemba
Akiwa kwenye ziara yake ya Ulaya, Diamond alienda Paris na kuingia studio na msanii huyo kurekodi wimbo huo alioshirikishwa. Hakusema awali kwakuwa kilichobainika kwenye safari hiyo ni kuingia studio na Fally Ipupa aliyemshirikisha.

Diamond amepost video inayowaonesha wawili hao wakiwa studio baada ya kurekodi wimbo. Wimbo huo unasikika kwenye video hiyo chini.
Previous Post Next Post