
Katika Mechi ya Kwanza iliyochezwa huko Kigali, Rwanda, Yanga iliitandika APR Bao 2-1 kwa Bao za Juma Abdul na Thaban Kamusoko.
Leo Yanga walianza vibaya kwa kupigwa Bao Dakika ya 4 tu lakini Donald Ngoma akasawazisha Dakika ya 28 na kuwaingiza Raundi ya mwisho ya mtoano ambayo watapambana na Mshindi kati ya Al Ahly ya Egypt na Recreativo de Libolo ya Angola ambazo nazo Leo zinacheza Mechi ya Pili huko Borg El Arab Stadium Mjini Alexandria Nchini Misri baada kutoka 0-0 huko Angola.
**Kwenye Mabano Jumla ya Mabao kwa Mechi mbili
Cnaps Sports (Madagascar) 2-1 Wydad Athletic Club (Morocco) [3-6]
Vitalo FC (Burundi) 2-1 Enyimba International FC (Nigeria) [3-6]
Young Africans (Tanzania) 1-1 Armee Patriotique Rwandaise FC (Rwanda) [3-1]
Tags
SPORTS NEWS