Watu 34 wanaotajwa kuwa ni Raia wa Nchi ya Ethopia, wanashikilwa na jeshi la polisi mkoani hapa (LINDI) kwa tuhuma za kuingia nchini kinyume cha sheria.
Afisa uhamiaji wa mkoa wa Lindi, Abdallah Towo ,amethibitisha kukamatwa watu hao. Ofisa huyo alisema watu hao walikamatwa mchana wakiwa wamejificha porini, katika mtaa wa Mmongo, Manispaa ya Lindi.
Towo amesema watu hao walikutwa katika eneo hilo wakiwa wamekaa na vifurushi vidogovido vikiwa na vyakula na maji.
"walikuwa wanakwenda wapi lakini walikutwa wamekaa kwenye pori hilo, mtaa wa Mmongo," alisema Towo.
Alisema taratibu za kuwafikisha mahakamani wahamiaji haramu hao zinashugulikiwa, Ambapo wakati wowote watafikishwa mahakamani.
Naye kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Lindi, David Mafwimbo alithibitisha kukamatwa watu hao, nakuongeza kusema walikutwa kwenye pori hilo kwenye korongo.
"taarifa hizo ni zakweli, watu hao walikuwa wanataka kwenda Afrika ya kusini wamekutwa na vibegi na Vifuko vidogo vidogo vya chakula,"aliongeza kusema Mafwimbo.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.