Unknown Unknown Author
Title: TANZANIA YATAJWA MIONGONI MWA MATAIFA 10 YANAYOKUWA HARAKA
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Balozi LIU GUIJIN TANZANIA imetajwa kuwa miongoni mwa mataifa kumi yanayokuwa kwa haraka duniani kutokana na kuwa na Amani na utulivu, ...
LIU GUIJIN
Balozi LIU GUIJIN

TANZANIA imetajwa kuwa miongoni mwa mataifa kumi yanayokuwa kwa haraka duniani kutokana na kuwa na Amani na utulivu, utawala bora pamoja na mwendelezo wa sera thabiti za maendeleo.

Hayo yamesemwa na balozi LIU GUIJIN aliyewahi kuwa balozi wa CHINA katika mataifa ya ZIMBABWE na AFRIKA KUSINI, wakati akifungua mjadala wa AMANI na MAENDELEO ambao umefanyika katika chuo kikuu cha BEIJING.

Kwa upande wake DR LAMIN SISSE aliyekuwa mshauri mkuu wa masuala ya kidiplomasia wa katibu mkuu wa zamani wa wa umoja wa mataifa KOFFI ANNAN, amesema imefika wakati kwa mataifa ya AFRIKA kuamua kusimama yenyewe bila kutegemea masaada wa mataifa mengine katika maendeleo.

Ameongeza kuwa matatizo ambayo mataifa mengi ya AFRIKA yanapitia ikiwemo vita za wenyewe kwa wenyewe iwe chachu ya kupata maendeleo.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top