Mwanamuziki Chigwele Che Mundugwao enzi za uhai wake.
Rais wa Shirikisho la Muziki Tanzania Ado Novemba, alisema marehemu alifikwa na umauti huo baada ya kufikishwa hospitalini akitokea Keko gerezani ambako alikuwa mahabusi.
“Marehemu Che Mundugwao alikuwa akisumbuliwa na tatizo la upungufu wa damu miezi miwili iliyopita, akiwa huko alipelekwa katika hospitali ya Amana na kugundulika na tatizo hilo. Mpaka sasa bado hatujafahamishwa chanzo cha kifo chake,” alisema Novemba.
Naye Makamu wa shirikisho hilo Samuel Mbwana alisema, “Che Mundugwao alilazwa katika hospitali ya Amana kwa kipindi cha miezi miwili kabla ya kurudishwa mahabusu na baadaye alipelekwa katika hospitali ya Muhimbili ambako alilazwa kwa muda kabla ya umauti kumfika leo saa moja asubuhi. Taarifa za mwisho za marehemu bado hatujazipata. Na ukizingatia alikuwa chini ya ulinzi hivyo bado hatujajua.”
Chigwele Che Mundugwao aliyekuwa ofisa Manunuzi wa Idara ya Uhamiaji na wenzake watatu walifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu Dar es Salaam mapema mwaka jana, wakikabiliwa na mashtaka manne likiwemo kosa la wizi wa Pasipoti 26.
Mungu aiweke roho ya marehemu mahali panapostahili. Amina.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.