Ikumbukwe kwamba Chrispine Mizengo Pinda na Adeline Ngugi wote wamehitimu pamoja katika chuo cha kimataifa cha Diplomasia kilichopo kurasini jijini Dar es Salaam amabapo walisoma Post Graduate in Management of Foreign Relations.
Marafiki wa karibu wa Chrispine na Adeline waliowakilisha wanafunzi wa chuo cha Diplomasia katika Hrusi hiyo wakifurahi Pamoja walipokuwa katika sherehe hiyo wakiongozwa na Khadija,Hassan ,Zitta,Lulu,Diana,Kennedy,Ngamanya,Mwanakatwe na Glady
Binti huyu mwenye gauni la bluu Lulu Rodgers (katikati) ndiye aliyedaiwa kumwaga chozi kwa furaha baada ya kuona wawili hao ambao ni marafiki zake wakifunga ndoa takatifu jana kwani anasema walikuwa wakitaniana sana kiasi kwamba anaamini ndoa yao itakuwa ya furaha na amani sana..