DANI ALVES AKATAA OFA YA KUSAINI MKATABA MPYA NA BARCELONA

Beki wa pembeni kutoka nchini Brazil, Daniel Alves da Silva na club ya Barcelona, amekataa ofa ya kuongezewa mkataba na klabu hiyo kwa ajili ya msimu ujao na wakala wake tayari amethibitisha hilo.
Daniel Alves da Silva
Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa na wakala wa beki huyo mwenye umri wa miaka 31, Dinorah Santa Ana, imeelezwa kwamba uongozi wa FC Barcelona huenda ukaanza mazungumzo ya kumsainisha mkataba mpya Dani Alves wakati wowote kabla ya mwishoni mwa msimu huu.

Dinorah Santa Ana ambaye alikuwa mke wa Dani Alves ameongeza kwamba suala hilo kwake analipa nafasi kubwa kutokana na kuamini kwamba kuna uwezekano wa pande hizo mbili zikafikia maamuzi na kusaini mkataba mpya.

Gazeti la Mundo Deportivo, limeripoti kwamba Santa Ana alikuwa na kikao kilichotumia muda wa saa mbili dhidi ya viongozi wa FC Barcelona usiku wa kuamkia jana kwa lengo la kufahamu mustakabali wa mchezaji wake kutokana na nafasi aliyo nayo hivi sasa huko Camp Nou.

Beki huyo wa zamani wa Sevilla amekuwa akihusishwa kuhamia Manchester United,Manchester City zote za England pamoja na PSG ya Ufaransa.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post