Unknown Unknown Author
Title: LICHA YA KUGOMEA ZOEZI LA UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MTAA, WAKAZI WA LUO NA MPEMBE WAKO TAABANI
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi , OLIVER VAVUNGE Wakazi wa Vijiji vya LUO na MPEMBE vilivyopo katika jimbo la ...
OLIVER VAVUNGE
Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi , OLIVER VAVUNGE

Wakazi wa Vijiji vya LUO na MPEMBE vilivyopo katika jimbo la MTAMA Halmashauri ya Wilaya ya LINDI VIJIJINI katika kata ya KIWALALA wameiomba serikali kuzipa Kipaumbele changamoto kubwa za ukosefu wa barabara pamoja na uhaba wa watumishi na vitendea kazi katika Zahanati ya Vijiji hivyo ili kuweza kupunguza madhara yanayojitokeza husuani kwa akina mama wajawazito pindi inapofika Muda wa Kujifungua.

Wakizungumza na Lindiyetu.com wakazi wa vijiji hivyo wameelezea namna ukosefu wa barabara inayounganisha maeneo hayo umekuwa ukiathiri kwa kiasi kikubwa shughuli mbalimbazi za kimaendeleo, ambapo pia wamesema kutokana na ukosefu wa huduma muhimu ikiwemo vifaa, na madawa muhimu katika Zahanati hiyo, inawalazimu kusafiri umbali mrefu hadi mjini kupata huduma hizo kwani mpaka sasa zahanati hiyo ina mtumishi mmoja tu anayehudumia wakazi wa eneo lote jambo linalohatarisha kwa kiasi kikubwa afya za wagonjwa hususani akina mama wajawazito pindi inapofika muda wa kujifungua.

Mganga wa zahanati ya Vijiji hivyo SOMOE RASHID amesema analazimika kufanya shughuli zote peke yake kutokana na kukosa wasaidizi ambao wamekuwa wakishindwa kuishi maeneo hayo kutokana na ugumu wa maisha ikiwemo changamoto kubwa ya ukosefu wa umeme na maji na hivyo kujikuta akifanya kazi peke yake na kukiri kuelemewa na idadi kubwa ya wagonjwa katika Hospitali hiyo ambapo pia amesema uchakavu wa vifaa vilivyopo katika hospitali hiyo imekuwa changamoto kubwa inayokabili vijiji hivyo.

Kwa upande wake afisa mtendaji wa Kijiji hicho AISHA LIPELA amesema changamoto za kijiji hicho zimekuwa zikiathiri kwa kiasi kikubwa maendeleo ya kijiji hicho ambapo amesema kijiji hicho mpaka sasa hakina uongozi wa kuchaguliwa na wananchi jambo linalokwamisha jitihada za maendeleo katika eneo hilo.

Disemba mwaka jana wakazi wa vijiji hivyo waligoma kushirki katika zoezi la kujiandikisha wala kupiga kura kushinikiza serikali kutafuta ufumbuzi wa haraka wa changamoto zinazo wakabili ambapo licha ya kufanya hivyo Hakuna jitihada zozote zilizofanyika.

Naye Mkurungenzi Mtendaji wa Halmashauri ya wilaya ya Lindi , OLIVER VAVUNGE ambaye ndiye msimamizi mkuu katika wilaya hiyo akapata fursa ya kuzungumza.

Aidha wananchi hao wamelalamikia juu ya ukosefu wa dawa na vifaa tiba katika zahanati zao za vijiji, jambo walilodai kwamba huathiri zaidi akina mama wajawazito inapofika wakati wa kujifungua.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top