Unknown Unknown Author
Title: MSANII MEZ B WA CHAMBER SQUAD AFARIKI DUNIA MJINI DODOMA LEO
Author: Unknown
Rating 5 of 5 Des:
Taarifa iliyotufikia mapema leo,inaeleza kuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la ‘Chamber Squad’ , Moses Bushagama ‘Mez B’ ...
mez b
Taarifa iliyotufikia mapema leo,inaeleza kuwa msanii wa muziki wa kizazi kipya kutoka kundi la ‘Chamber Squad’, Moses Bushagama ‘Mez B’, amefariki dunia leo asubuhi huko Mkoani Dodoma baada ya kusumbuliwa na Homa ya mapafu kwa muda mrefu.

 Taarifa ya kifo cha Mez B zimethibitishwa na mama yake mzazi, na kwamba alikuwa amelazwa kwenye Hospitali ya Mwananchi.

Mez B amewahi kulazwa na kuruhusiwa mara kadhaa katika hospitali ya Dodoma na hivi karibuni alizidiwa na kulazwa mkoani humo mpaka umauti ulivyompata.

Baadhi ya nyimbo alizowahi kuimba Mez B ni pamoja na ‘Fikiria’, ‘Kama Vipi’, ‘Kikuku’, ‘Shemeji’ ‘Nimekubali’ pamoja na ‘Ghetto langu’ aliyoshirikishwa na Marehemu Albert Mangwea.

Huyu ni msanii wa pili kufariki kutoka kundi la chamber squad. Miaka miwili iliyopita kundi hilo liliomboleza kifo cha mwenzao Albert Mangwea ‘Ngwea’ huku Mez B akiwa mstari wa mbele wakati wa mazishi yake.

Mungu ailaze roho yake mahali pema peponi.

About Author

Advertisement

Post a Comment Blogger

Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii

Note: Only a member of this blog may post a comment.

 
Top