MANCHESTER UNITED YAPAA HADI NAFASI YA TATU, BAADA YA KUIFUNGA SOUTHMPTON NYUMBANI

Baada ya Chelsea kupoteza mchezo kwenye ligi dhidi ya Newcastle jumamosi, Arsenal kudhalilishwa na Stoke City, huku Man City na Liverpool wakishinda – leo ilikuwa zamu ya Man United kucheza dhidi ya Southmpton.
RVP
Matokeo ya mchezo huo uliopigwa kwenye uwanja wa St Mary umemalizika kwa United kushinda mechi ya 5 mfululizo na kufanikiwa kushika na nafasi ya tatu kwenye ligi, mara ya kwanza tangu Sir Alex Ferguson alipokuwa Kocha wao.
Magoli mawili ya Robin Van Persie yalitosha kuifanya United kuwaondoa West Ham katika nafasi ya 3.
Pelle aliifungia Southampton goli la
Kufutia machozi kwenye mchezo huo ambao United hawakucheza vizuri.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post