TETESI ZA USAJILI:: MAN UNITED WAMWAGA PAUNDI MILIONI 20 KWA TONI KROOS BAADA YA VAN GAAL KUBARIKI

Toni kroos
United wamekubaliana na Bayern Munich kuuziana Toni Kroos

MANCHESTER United amekubaliana dili la kumsajili kiungo wa Bayern Munich,Toni Kroos na sasa wanajipanga kuiwinda saini ya mchezaji mwenzake, Mholanzi Arjen Robben.

Kross alikubaliana na ofa ya paundi milioni 20 na aliyekuwa kocha wa Manchester United, David Moyes na mrithi wake ambaye aliyewahi kuwa kocha wa Bayern Munich, Louis Van Gaal amebariki dili hilo kuendelea.


Kroos, 24, aling`ara wakati wa utawala wa Van Gaal katika klabu ya Bayern na bado anahitaji kufanya kazi na kocha wake wa zamani.

Arjen Robben
Yupo kwenye rada: United kwasasa wapo katika mawindo ya kumnasa nyota wa Bayern, Arjen Robben
 Louis Van Gaal
Tabasamu tu: Kocha wa Uholanzi, Louis Van Gaal akitasamu katika mazoezi ya timu yake mjini Lagos nchini Ureno.

Robben ni mchezaji wa kwanza kusajiliwa na Van Gaal wakati akiwa Bayern kwa ada ya uhamisho wa paundi milioni 20 kutokea klabu ya Real Madrid mwaka 2009.
Siku za karibuni winga huyo mwenye miaka 20 alisaini mkataba wa miaka mitatu na Bayern, lakini haimvunji moyo Van Gaal ambaye atafanya kazi na Robben katika fainali za kombe la dunia mwaka huu nchini Brazil.

Inafahamika kuwa United wamekubaliana dili la paundi milioni 27 ili kuinasa saini ya beki wa kushoto wa Southampton, Luke Shaw na beki wa kati wa Borussia Dortmund, Mats Hummels yupo katika mipango ya Van Gaal.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post