Jumla ya
wanafunzi 111 wamepata mimba kwa kipindi cha mwaka 2012/13 katika
shule za msingi na sekondari mkoani Lindi na 1405 kati ya 8399 waliochaguliwa
kujiunga elimu ya sekondari mwaka huu mkaoni Lindi hawajafika kwenye shule
hizo kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo utoro,
Hayo
yamebainishwa na afisa elimu mkoa Silas Semaluku alipokuwa anazungumza na
wadau wa elimu kwenye mkutano wa wadau wa Elimu mkoani Lindi.
Semaluku alisema
mkoa una kabiliwa na changamoto kubwa za watoto kupata mimba kutokana na sababu mbalimbali ikiwemo tamaa kwa watoto
wakike kuwa na vitu vya thamani ambazo zimeanza kufanyiwa kazi , na idara ya
elimu pamoja na wazazi,
Alisema wilaya
Lindi inaongoza kwa kuwa na watoto wengi waliopata ujauzito ambao 48 ikifuatia
wilaya Kilwa 23, Nachingwea 18, Ruangwa 14, Liwale 6 na manispaa ya Lindi
2.
Semaluku alisema
kuwa mkoa ulipangiwa wanafunzi 8,399 kati yao wasichana 4,078 na wavulana 4,321
lakini waliofika shuleni hadi sasa ni 6,994 pia wanafunzi 1,405 hawajafika shule
hadi sasa kati yao wavulana 720 na wasichana 685.
Alifanunua kuwa
wanafunzi halmashauri ya wilaya Lindi kuna wanafunzi 327 wahajafiki shule hadi
sasa, Liwale wanafunzi 230, Kilwa 200 Ruangwa 351 wilaya ya Nachingwea 226 huku
Manispaa ya Lindi ikiwa na wanafunzi 69.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.