Rapa mpuerto rico, Fat Joe amewashitua watu wengi kwa muonekano mpya aliokuwa nao hivi sasa baada ya kukaa nyuma ya nondozz ‘jela’ miezi minne kwa kosa la kukwepa kulipa kodi. Mkali huyo wa ngoma ya ‘Ballin’ amepungua paundi 200 ambazo ni sawa na kilo 90 na kumfanya aonekana tofauti na alivyokuwa hapo awali.
Fat Joe kabla na baada ya kupungua.
Hata hivyoJoe amemtupia lawama zote msimamizi wake wa masuala ya fedha kwa kuzembea kulipa kodi kwa muda uliotakiwa na kumlaumu kutoa taarifa kwa polisi ambao walimsweka ndani kwa muda wa miezi 4.
Mh! Kweli jela shule, miezi minne kapoteza kilo 90 bila kupenda, je angekaa mwaka mzima??? i think tungemsahau kabisa
Kwa sasa Fat Joe amejipanga kuja na kipindi cha televisheni kitakachokuwa kikirushwa hewani na kituo cha utangazaji cha ABC hivi karibu. Swali, Je rapa huyo atabadili jina lake kwa kutoa jina la Fat ambalo alilipata kutokana na unene wa kupindukia aliokuwa nao? Wacha muvi iendelee.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.