MKUU WA WILAYA YA KIBONDO VENANCE MWAMOTO AMTAKIA KILA LAKHERI MGOMBEA UBUNGE JIMBO LA KALENGA,GODFREY MGIMWA

clip_image001Pichani Kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Kibondo,Mkoani Kigoma Mh.Venance Mwamoto akisalimiana na kumtakia kila la kheri mgombea Ubunge kwa tiketi ya chama cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Godfrey William Mgimwa, katika mchaka mchaka wake wa kampeni za uchaguzi mdogo wa Jimbo la Kalenga, Iringa Vijijini na hatimae kuibuka mshindi.

Uchaguzi wa jimbo hilo unatarajiwa kufanyika mnamo tarehe 16 machi 2014, ambapo wananchi wa jimbo hilo wameombwa kujitokeza kwa wingi kushiriki zoezi hilo la upigaji kura na hatimae kumchagu kiongozi (Mbunge) wamtakae kwa maendeleo ya jimbo lao. Aidha Vyombo vya Usalama pia vimetoa rai kwa Wananchi kuwa watulivu kwa wakati wote wa kampeni na uchaguzi, ili kuhakikisha amani na utulivu vinatawala muda wote pasi na vurugu. 

clip_image001[5]"Kila lakheri Mdogo wangu"-Venance Mwamoto.

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post