Inaitwaje hii: Mario Balotelli ameweka kwenye akaunti yake ya Twitter jana usiku picha hii ya mtindo wake mpya unyoaji
MSHAMBULIAJI wa AC Milan, Mario Balotelli amepamba vichwa vya habari tena baada ya kuibuka na mtindo mpya wa unyoaji kichwani.
Mshambuliaji huyo wa Italia jana usiku aliposti picha za mnyoo wake mpya katika akaunti yake ya Twitter.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 23 ameonekana wa kipekee kwa mnyoo huo hatari. "Nimemaliza kunyoa, sasa naenda zangu kulala," hayo ndiyo maneno yaliyoambatana na picha hizo.
Balotelli amewahi kuweka mitindo hii ya nywele hapo kabla
Mitindo mingine ya nywele ya Balotelli hapo awali
Tags
SPORTS NEWS