MAPINDUZI CUP-MIAKA 50: NUSU FAINALI, SIMBA USO KWA USO NA URA YA UGANDA

clip_image001Mapinduzi Cup, Kombe la Kusheherekea Miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar, Usiku huu limemaliza Mechi zake za Robo Fainali na Mechi za Nusu Fainali zitashindaniwa na Timu toka Uganda dhidi ya Timu kutoka Tanzania Bara katika Mechi zote mbili.

Mabigwa Watetezi, Azam FC, wao walitinga Nusu Fainali kwa kuichapa Clove Stars, Kombaini ya Pemba, Bao 2-0, URA ya Uganda kuitungua KMKM 1-0, Tusker ya Kenya na KCC ya Uganda kutoka 0-0 katika Dakika 90 na KCC kuibuka Mshindi kwa Mikwaju ya Penati.

Simba, wakicheza Mechi ya mwisho ya Robo Fainali Uwanjani Amaan Saa mbili Usiku huu waliichapa Chuoni ya Zanzibar Bao 2-0, Bao zote zikifungwa na Ramadhan Singano.

Nusu Fainali, ambazo zitachezwa Ijuma Januari 10, Azam FC itaivaa KCC na Simba kupambana na URA.

Fainali ni Jumatatu Januari 13 kwenye Uwanja wa Amaan Jijini Zanzibar.

RATIBA/MATOKEO: ROBO FAINALI

Jumatano Januari 8, Gombani Stadium, Pemba

KMKM 0 URA 1

Azam FC 2 Clove Stars 0

Amaan Stadium

Tusker 0 KCC 0 [KCC imesonga kwa Penati 4-3]

Simba 2 Chuoni 0

NUSU FAINALI: Ijumaa Januari 10

SAA 10 JIONI: Azam FC v KCC

SAA 2 USIKU: URA v Simba

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post