Watu watatu wanaoshukiwa kuwa wanamgambo wa al-Shabaab walikufa baada ya kifaa cha mlipuko walichokuwa wakikitega kulipuka kwenye wilaya ya Wadajir, Mogadishu, siku ya Jumanne asubuhi (tarehe 23 Julai), iliripoti Redio Bar-Kulan inayofadhiliwa na Umoja wa Mataifa.
Mlipuko huo ulilitikisa jengo la karibu na mwanamke mmoja alijeruhiwa, ingawa haikuwa wazi ikiwa alikuwamo ndani ya jengo hilo wakati bomu lilipolipuka.
Vikosi vya usalama vya Somalia vililifunga haraka eneo hiyo na kuanza upelelezi.
Post a Comment Blogger Facebook
Toa Maoni Yako Kuhusu habari Hii
Note: Only a member of this blog may post a comment.