MOURINHO: NI KWELI TUMETUMA OFA KWA MAN UNITED - SASA TUMEWAACHIA WAAMUE

JOSE MOURINHO amesisitiza kwamba sasa ni uamuzi wa mwisho kuhusu usajili wa Wayne Rooney umebaki mikononi mwa klabu ya Manchester United.

Chelsea leo mchana ilithibitisha kwamba wametuma ofa rasmi ya kumsajili Rooney lakini United wameikataa
Lakini muda mfupi uliopita Mourinho amethibitisha kwamba Rooney ndio mchezaji pekee anayemhitaji kwenye kikosi chake.
"Nadhani kila kitu kipo wazi sasa - sio siri tena. Ofa rasmi imetumwa lakini ilikuwa ya kiasi cha fedha na haikuhusisha mchezaji yoyote. Tunamhitaji mchezaji. Tumetuma ofa na sasa hatuna cha kusema zaidi. Tumewaachia Manchester United waamue.”

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post