BreakingNEWS: KIU Yafungiwa Kutoa Mastars na PhD

Tume ya VyuoVikuu Tanzania (TCU) hivi punde imekitaka Chuo Kikuu cha Kimataifa cha Kampala (KIU) kusimamisha mara moja kufundisha au kutoa mafunzo ya Shahada ya Juu (Postgraduate), Shahada ya Uzamili (Masters) na Shahada za Uzamivu (PhD) katika kampasi ya Dar es Salaam, Tanzania.
KIU imeamriwa kusimamisha kutoa shahada hizo kuanzia LEO hawana wahadhiri wa kutosha wenye sifa stahili jambo ambalo ni kinyume cha taratibu.
Taarifa imetolewa na Katibu Mtendaji wa TCU, pia KIU imeamriwa kuzungumza na kushirikiana vizuri na wanafunzi wote waliodahiliwa katika kozi zilizotajwa hapo juu ili wahamie kwenye  vyuo  vingine vyenye  idhibati ya kutoa  mafunzo  hayo.
“Tume haitatambua shahada yeyote ya uzamili au uzamivu itakayotolewa na chuo hicho ambao watasoma katika kampasi ya Dar es Salaam, Tanzania.
“Chuo cha KIU Kampasi ya Dar es Salaam kina ithibati na kitaendelea kutoa mafunzo ya shahada ya kwanza (Bachelors), Diploma au vyeti zilizopitishwa na TCU kwa mujibu wa Ithibati husika tuu,” imesema sehemu ya taarifa iliotolewa na Katibu Mtendaji wa TCU.
Uamuzi huo umefikiwa  na tume hiyo katika mkutano wake wa hivi karibuni uliofanyika jijini Dar es Salaam.

habari zaidi bofya hapa

Post a Comment

Hii ni Blog kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Nchi yetu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...

Previous Post Next Post